YouVersion Logo
Search Icon

Ezra UTANGULIZI

UTANGULIZI
Vitabu vya Mambo ya Nyakati, hiki cha Ezra, pamoja na kitabu kinachofuata cha Nehemia, vyote vimetokana na mazingira yaleyale. Kitabu hiki kimepewa jina la mtu maarufu aitwaye Ezra ambaye alikuwa mmoja wa viongozi wa Wayahudi wakati waliporudi kutoka uhamishoni.
Kitabu chenyewe chaanza na tangazo rasmi lililotolewa na mfalme Koreshi wa Persia kuwaruhusu watu wa Israeli warejee makwao kujenga upya hekalu la Yerusalemu (sura 1). Kisha tunapewa idadi kubwa ya hao wakimbizi ambao walianza safari ya kurudi makwao (sura 2). Shughuli yao ya kwanza huko Yerusalemu ilikuwa kupata ile madhabahu ya dhabihu na kuanzisha tena ibada kwa Mungu (sura 3). Matayarisho hayo hata hivyo yalisababisha upinzani kutoka kwa maadui na kwa sababu hiyo kukawa na barua kadha wa kadha kwa wakuu wa Persia ambao walithibitisha kwamba idhini ilikuwa imekwisha tolewa (sura 4–6).
Sehemu ya pili ya kitabu inaeleza jinsi kuhani Ezra, akiwa ametumwa na mfalme Artashasta, alivyofufua na kurekebisha maisha ya dini huko Yerusalemu (sura 7–10).
Ujumbe wa kitabu cha Ezra unasisitiza na kutilia mkazo umuhimu wa imani na maisha mema na safi.

Currently Selected:

Ezra UTANGULIZI: BHND

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy