Ufunuo 12:14-16
Ufunuo 12:14-16 SWC02
Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu. Basi yule nyoka akatokeza maji kwa uwingi ndani ya kinywa chake, nayo yakatelemuka kama muto nyuma ya yule mwanamuke kusudi yapate kumupeleka. Lakini udongo ukamusaidia yule mwanamuke; ukabomoka kama vile kinywa na kumeza ule muto uliotoka katika kinywa cha yule nyoka.





