YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 42

42
SEHEMU YA PILI
(Zaburi 42–72)
Maombi ya mukimbizi
1 # 42.1 Katika maandiko mengi ya kiebrania, Zaburi 42 na 43 ni zaburi moja. Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Wakora.
2Kama pongo anavyotamani maji ya kijito,
ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!
3Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima.
Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?
4Machozi ni chakula changu muchana na usiku;
ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”
5Katika huzuni yangu, ninakumbuka
jinsi nilivyokwenda na kundi la watu
na kuwaongoza kwenda katika nyumba ya Mungu
wakipiga vigelegele vya shukrani,
kundi la watu likifanya sherehe!
6Mbona ninaugua hivyo katika moyo?
Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu?
Nitamutumainia Mungu,
maana nitamusifu tena
yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.
7Roho yangu imeregea kabisa,
kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu,
kutoka katika eneo la Yordani,
kutoka mulima Hermoni na Mizari.
8Mafuriko juu ya mafuriko yananguruma,
mawimbi na zoruba yako vinanifunika.
9Yawe atanijalia wema wake muchana;
nami nitamwimbia wimbo wa sifa usiku,
nitamwomba Mungu anayenipa uzima.
10Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu:
“Kwa nini umenisahau?
Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza
kwa kuteswa na adui yangu?”
11Nimepondekana kwa ajili ya matukano yao,
wanaponiuliza kila siku:
“Mungu wako, yupo wapi?”
12Mbona ninaugua hivyo katika moyo?
Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu?
Nitamutumainia Mungu,
maana nitamusifu tena Mungu,
anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

Currently Selected:

Zaburi 42: SWC02

Highlight

Copy

Compare

Share

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in