Zaburi 41
41
Maombi ya mugonjwa
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
2Heri mutu anayeshugulikia masikini;
Yawe atamwokoa wakati wa shida.
3Yawe atamulinda na kuchunga uzima wake,
naye atafanikiwa katika inchi;
hatamwacha katika makucha ya waadui zake.
4Yawe atamusaidia anapokuwa mugonjwa,
atamuponyesha magonjwa yake yote.
5Nami nilisema: “Unirehemu, ee Yawe,
uniponyeshe, maana nimekukosea.”
6Waadui zangu wanasema hivi vibaya juu yangu:
“Atakufa wakati gani kusudi jina lake lisahauliwe!”
7Wananitembelea bila kuwa na nia njema,
wanawaza mabaya juu yangu,
wanapofika inje wanawatangazia wengine.
8Wote wanaonichukia wananongoneza juu yangu;
wananiwazia mambo mabaya.
9Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua;
hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”
10Hata rafiki yangu wa moyo niliyemwamini,
rafiki aliyechangia chakula nami,
amegeuka kunishambulia! #Ang. Mat 26.23; Mk 14.18; Lk 22.21; Yn 13.18
11Ee Yawe, unionee huruma!
Uniponyeshe, nami nitawalipiza kisasi.
12Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami,
waadui zangu wasipopata ushindi juu yangu.
13Wewe unaniimarisha katika ukamilifu;
utanichunga mbele yako milele.
14Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe,
tangu milele na hata milele!
Amina! Amina! #Ang. Zab 106.48
Currently Selected:
Zaburi 41: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Zaburi 41
41
Maombi ya mugonjwa
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
2Heri mutu anayeshugulikia masikini;
Yawe atamwokoa wakati wa shida.
3Yawe atamulinda na kuchunga uzima wake,
naye atafanikiwa katika inchi;
hatamwacha katika makucha ya waadui zake.
4Yawe atamusaidia anapokuwa mugonjwa,
atamuponyesha magonjwa yake yote.
5Nami nilisema: “Unirehemu, ee Yawe,
uniponyeshe, maana nimekukosea.”
6Waadui zangu wanasema hivi vibaya juu yangu:
“Atakufa wakati gani kusudi jina lake lisahauliwe!”
7Wananitembelea bila kuwa na nia njema,
wanawaza mabaya juu yangu,
wanapofika inje wanawatangazia wengine.
8Wote wanaonichukia wananongoneza juu yangu;
wananiwazia mambo mabaya.
9Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua;
hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”
10Hata rafiki yangu wa moyo niliyemwamini,
rafiki aliyechangia chakula nami,
amegeuka kunishambulia! #Ang. Mat 26.23; Mk 14.18; Lk 22.21; Yn 13.18
11Ee Yawe, unionee huruma!
Uniponyeshe, nami nitawalipiza kisasi.
12Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami,
waadui zangu wasipopata ushindi juu yangu.
13Wewe unaniimarisha katika ukamilifu;
utanichunga mbele yako milele.
14Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe,
tangu milele na hata milele!
Amina! Amina! #Ang. Zab 106.48
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.