Zaburi 28
28
Kuomba musaada
1Zaburi ya Daudi.
Ninakulilia,
ee Yawe!
Ewe kikingio changu, usikuwe kama kiziwi kwangu.
Usikuwe kama haunisikilizi,
nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.
2Sikiliza sauti ya ombi langu,
ninapokulilia unisaidie,
ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.
3Usiniazibu pamoja na watu wabaya,
wale watenda maovu wanaosema vizuri na wenzao,
kumbe wanajaa ubaya ndani ya moyo.
4Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao,
kufuatana na maovu waliyotenda.
Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao wenyewe;
uwatendee yale wanayostahili. #Ang. Ufu 22.12
5Hawashuguliki na matendo ya Yawe;
hawatambui mambo aliyofanya.
Kwa sababu hiyo atawabomoa,
wala hatawajenga tena upya.
6Atukuzwe Yawe,
maana amesikiliza ombi langu.
7Yawe ndiye nguvu na ngao yangu;
tegemeo la moyo wangu ni kwake.
Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote;
kwa wimbo wangu ninamushukuru.
8Yawe ni nguvu ya watu wake;
yeye ni kimbilio la mufalme aliyemuchagua.
9Ee Mungu, uwaokoe watu wako;
uwabariki watu hao wanaokuwa mali yako.
Ukuwe muchungaji wao na kuwalinda milele.
Currently Selected:
Zaburi 28: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.