Zaburi 23
23
Mungu ni muchungaji wangu
1Zaburi ya Daudi.
Yawe ni muchungaji wangu;
sitapungukiwa na kitu.
2Ananipumzisha kwenye majani mabichi;
ananiongoza kando ya maji matulivu,
3na kuirudishia nafsi yangu nguvu mupya.
Ananiongoza katika njia sawa
kwa utukufu wa jina lake.
4Hata nikipita katika bonde la giza kubwa,
sitaogopa hatari yoyote,
maana wewe, ee Yawe, ni pamoja nami;
gongo lako na fimbo yako vinanipa moyo.
5Umenitayarishia karamu mbele ya waadui zangu.
Umekipakaa kichwa changu mafuta.
Kikombe changu umekijaza tele.
6Kweli, uzuri na wema wako vitakuwa pamoja nami
siku zote za maisha yangu;
nami nitakaa katika nyumba ya Yawe milele.
Currently Selected:
Zaburi 23: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.