Zaburi 20
20
Kuomba ushindi
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
2Yawe akujibu unapokuwa katika taabu;
jina la Mungu wa Yakobo likulinde.
3Akupelekee musaada kutoka katika hekalu lake;
akukinge tokea kwenye mulima Sayuni.
4Akumbuke sadaka zako zote;
akubali sadaka zako za kuteketezwa.
5Akujalie unayotamani ndani ya moyo wako,
afanikishe mipango yako yote.
6Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako;
tutainua bendera kwa kutukuza jina la Mungu wetu.
Yawe akutimizie mapenzi yako yote!
7Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua,
atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni;
kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.
8Wamoja wanajivunia magari ya vita, wengine farasi wao.
Lakini sisi tunajivunia Yawe, Mungu wetu.
9Hao wanajikwaa na kuanguka;
lakini sisi tunasimama na kuimarika.
10Ee Yawe, umujalie mufalme ushindi,
utujibu wakati tunapokuomba.
Currently Selected:
Zaburi 20: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.