Zaburi 150
150
Mumusifu Mungu!
1Mumusifu Mungu katika pahali pake patakatifu,
mumusifu juu mbinguni kwenye uwezo wake!
2Mumusifu kwa sababu ya matendo yake makubwa,
mumusifu kwa ajili ya utukufu wake mukubwa!
3Mumusifu kwa mulio wa baragumu,
mumusifu kwa zeze na kinubi!
4Mumusifu kwa ngoma na michezo,
mumusifu kwa filimbi na kinanda!
5Mumusifu kwa matoazi ya sauti kubwa,
mumusifu kwa matoazi yenye kuvuma sana!
6Kila kiumbe chenye uzima kimusifu Yawe!
Mumusifu Yawe!
Currently Selected:
Zaburi 150: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.