Mezali 1
1
Shabaha ya mezali
1Hizi ni mezali za Solomono mwana wa Daudi mufalme wa Israeli. #Ang. 1 Fal 4.32 2Zitawawezesha watu kujua hekima na mafundisho, na kufahamu misemo yenye maana kubwa. 3Zitawafundisha watu matendo ya hekima, haki, usawa, na sheria ya Mungu. 4Zitawaerevusha wajinga, zitawapa vijana maarifa na akili. 5Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi. 6Wataweza kuelewa mezali na maana iliyofichwa, watayaelewa maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.
7Kumwogopa Yawe ni musingi wa maarifa,
lakini wapumbafu wanazarau hekima na mafundisho. #Ang. Yobu 28.28; Zab 111.10; Mez 9.10
Maonyo kwa vijana
8Mwana wangu, sikiliza mafundisho ya baba yako,
wala usizarau mashauri ya mama yako;
9hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako,
kama mukufu katika shingo yako.
10Mwana wangu, usikubali kushawishiwa na wenye zambi.
11Wakisema: “Twende kuvizia mutu na kumwua;
kuja tuwashambulie wasiokuwa na kosa!
12Tutawameza wakiwa wazima kama kuzimu,
watakuwa kama wale wanaoshuka katika shimo.
13Tutajitwalia mali zote za bei kali,
tutazijaza nyumba zetu vitu tulivyonyanganya.
14Kuja na ushirikiane nasi,
vyote tutakavyopata tutagawanyana.”
15Wewe mwana wangu usiandamane nao,
uzuie muguu wako usifuatane nao.
16Maana wao wako mbio kutenda maovu,
haraka zao zote ni za kumwanga damu.
17Mutego unaotegwa na ndege akiona,
mutego ule unategwa bure.
18Wao wanavizia na kujiangamiza wao wenyewe,
wanatega mutego wa kujinasa wao wenyewe.
19Ndizo njia za wanyanganyi;
maisha yao yananyanganywa.
Hekima inaita
20Hekima inapiga kelele katika barabara,
inaita kwa sauti kubwa katika viwanja; #Ang. Mez 8.1-3
21inaita kwenye masanganjia,
inaita kwenye milango ya muji:#1.21 milango ya muji: hapa ndipo pahali watu walipokutana kwa kutatua matatizo na maneno yao.
22“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga?
Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao,
na wapumbafu kuchukia maarifa?
23Musikilize maonyo yangu;
nitawamiminia mawazo yangu,
nitawajulisha maneno yangu.
24“Nimewaita nanyi mumekataa kusikiliza,
nimewanyooshea mukono mukuje nanyi hamukujali,
25mumetupilia mashauri yangu yote,
mumezarau maonyo yangu.
26-27Kwa sababu hiyo,
woga utakapowapata kama zoruba,
hasara yenu itakapowatokea kama upepo mukali,
taabu na huzuni vitakapowapata,
nitachekelea hasara yenu na kuwasimanga.
28Halafu mutaniita lakini sitaitika;
mutanitafuta kwa bidii lakini hamutanipata.
29“Muliyachukia maarifa,
wala hamukuchagua kumwogopa Yawe,
30mulikataa shauri langu,
mukazarau maonyo yangu yote.
31Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu,
mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.
32Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao,
wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.
33Lakini mutu anayenisikiliza atakaa salama,
atatulia bila kuogopa mabaya.”
Currently Selected:
Mezali 1: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.