Nehemia UTANGULIZI
UTANGULIZI
Kitabu hiki ni mufululizo wa kitabu kilichotangulia, ni kusema Ezra. Nehemia aliishi wakati wa Ezra na alikuwa musimamizi mukubwa katika utawala wa Artasasta, mufalme wa Persia. Yeye alipata ruhusa kutoka kwa mukubwa wake arudi Yerusalema ajishugulishe na kutengeneza maisha ya siasa, uchumi na jamii (sura 1.1–2.10). Mara tu alipofika kule, ingawa alikutana na upinzani kutoka kwa waadui wamoja, aliungwa mukono na wamoja kati ya wanainchi wenzake wakajenga kuta za Yerusalema (sura 2.11–7.72). Nehemia na Ezra walikuwa pale wakati wa mukutano mukubwa wa kidini ambamo Ezra alihutubia juu ya sheria ya Mungu.
Watu walirudilia tena maagano yao kwa Mungu (sura 8.1–10.40). Nyuma ya kutoa mipango mbalimbali iliyoelekea hasa mambo ya siasa, Nehemia akasimamia muzinduo wa kuta zilizojengwa upya (11.1–12.43), kisha akaendelea na mambo mengine ya matengenezo ya dini (sura 12.44–13.31).
Currently Selected:
Nehemia UTANGULIZI: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.