YouVersion Logo
Search Icon

Matayo 3

3
Mahubiri ya Yoane Mubatizaji
(Mk 1.1-8; Lk 3.1-18; Yn 1.19-28)
1Katika siku zile Yoane Mubatizaji alitokea akihubiri katika jangwa la Yudea 2akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”
3Yoane ndiye yule Mungu aliyemutaja kwa njia ya nabii Isaya akisema:
“Sauti inatangaza katika jangwa:
‘Mutengeneze njia ya Bwana,
munyooshe pahali atakapopita!’ ”
4Yoane alikuwa akivaa nguo iliyotengenezwa na manyoya ya ngamia na mukaba wa ngozi katika kiuno. Naye alikuwa akikula nzige na asali ya pori. 5Watu wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea, nao waliokaa fasi zote pembeni ya muto Yordani walimufikia. 6Waliungama zambi zao, naye Yoane aliwabatiza katika muto Yordani.
7Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia? 8Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. 9Musijifikiri kwamba munaweza kujidai tu kuwa Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu! 10Shoka limekwisha kuwekwa tayari kwenye mashina ya miti. Kila muti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto. 11Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu. 12Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”
Ubatizo wa Yesu
(Mk 1.9-11; Lk 3.21-22)
13Wakati ule Yesu akatoka Galilaya na kufika kwenye muto Yordani, akamwendea Yoane kusudi abatizwe naye. 14Lakini Yoane akamukatalia, akimwambia: “Ni mimi ninayepaswa kubatizwa nawe; namna gani unakuja kwangu?” 15Lakini Yesu akamujibu: “Ukubali kufanya hivi sasa. Kwa maana ni kwa njia hii tutatimiza mambo yote yanayokuwa ya haki mbele ya Mungu.”
Basi Yoane akakubali. 16Yesu alipokwisha kubatizwa na kutoka ndani ya maji, mara moja mbingu zikafunguka, naye akamwona Roho wa Mungu akishuka kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake. 17Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”

Currently Selected:

Matayo 3: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy