YouVersion Logo
Search Icon

Walawi 12

12
Kuwatakasa wanawake kisha kuzaa
1Yawe akamwambia Musa: 2Uwaambie watu wa Israeli hivi: Mwanamuke akipata mimba na kuzaa mutoto mwanaume, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba sawa vile anavyokuwa kwa wakati wake wa ugonjwa wa mwezi. 3Mutoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane. #Ang. Mwa 17.12; Lk 2.21 4Kisha mama wa mutoto ataendelea kuwa muchafu kwa muda wa siku makumi tatu na tatu. Wakati huo, asiguse chochote kilichotakaswa wala kuingia Pahali Patakatifu mpaka siku za kutakasika kwake zitakapotimia. 5Lakini, kama amezaa mutoto mwanamuke, basi, atakuwa muchafu kwa muda wa majuma mawili kama vile inavyokuwa kwa wakati wa ugonjwa wake wa mwezi. Ataendelea katika kutakasika kwake kwa muda wa siku makumi sita na sita.
6Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, ikuwe amepata mutoto mwanaume au mwanamuke, atamuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano mwana-kondoo wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kitoto cha njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya zambi. 7Kuhani atamutolea mbele ya Yawe na kumufanyia huyo mama ibada ya upatanisho mbele ya Yawe. Hivyo huyo mwanamuke atakuwa safi kwa ajili ya kutokwa na damu yake. Hii ni sheria inayoelekea mwanamuke yeyote anayezaa mutoto mwanaume au mwanamuke.
8Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi. #Ang. Lk 2.24

Currently Selected:

Walawi 12: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in