YouVersion Logo
Search Icon

Yoshua 24

24
Waisraeli wanaamua kumutumikia Yawe
1Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu. 2Yoshua akawaambia watu wote: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Hapo zamani, wazee wenu waliishi ngambo ya muto Furati, wakaitumikia miungu mingine. Muzee mumoja aliitwa Tera, baba ya Abrahamu na Nahori. #Ang. Mwa 11.27 3Mimi Mungu nilimwondoa babu yenu Abrahamu kutoka kule ngambo ya muto Furati na kumuleta hapa Kanana, ambako nilimupatia wazao wengi. Nilimupa Isaka, #Ang. Mwa 12.1-9; 21.1-3 4naye Isaka nikamupa Yakobo na Esau. Nilimupa Esau milima ya Seiri airizi. Lakini Yakobo na watoto wake walikwenda Misri. #Ang. Mwa 25.24-26; 36.8; 46.1-7; Kumb 2.5 5Nyuma nikawatuma Musa na Haruni, nikailetea inchi ya Misri mapigo, na kisha nikawatoa ninyi katika inchi ile. #Ang. Kut 3.1–12.42 6Niliwatoa wazee wenu kutoka Misri na kuwaleta mpaka kwenye bahari Nyekundu. Wamisri waliwafuatilia wakiwa na magari na waaskari wapanda-farasi. #Ang. Kut 14.1-31 7Waisraeli waliponililia mimi Yawe, niliweka giza kati yao na Wamisri na kuifanya bahari iwafunike Wamisri. Ninyi wenyewe mulijionea yale niliyowatendea Wamisri. Muliishi katika jangwa muda murefu. 8Kisha niliwaongoza mpaka katika inchi ya Waamori ambao waliishi upande mwingine wa muto Yordani. Walipigana nanyi, lakini mimi niliwapa ushindi juu yao mukawaangamiza na kuiteka inchi yao. #Ang. Hes 21.21-35 9Naye Balaka mwana wa Sipori, mufalme wa Moabu, akakuja na kuwashambulia Waisraeli. Akamwalika Balama mwana wa Beori akuje kuwalaani ninyi. #Ang. Hes 22–24 10Lakini mimi sikumusikiliza Balama, naye akawabariki, nami nikawaokoa ninyi toka mikono ya Balaka. #Ang. Hes 22–24 11Halafu mukavuka muto Yordani, mukafika Yeriko. Wakaaji wa Yeriko walipigana nanyi, vilevile na Waamori, Waperizi, Wakanana, Wahiti, Wagirgasi, Wahivi na Wayebusi. Hao mimi nikawatia katika mikono yenu. #Ang. Yos 3.14-17; 6.1-21 12Nilituma nyuki mbele yenu ambazo ziliwafukuza wafalme wawili wa Waamori. Hamukufanya yale kwa kukamata mapanga wala mishale yenu. #Ang. Kut 23.28; Kumb 7.20
13“Niliwapa mashamba ambayo hamukukuwa mumeyalima, na miji ambayo hamukuijenga ambamo sasa munaishi, na kula matunda ya mizabibu na mizeituni ambayo hamukuipanda. #Ang. Kumb 6.10-11
14“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe. 15Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”
16Halafu watu wakamujibu: “Hatutaweza hata kidogo kumwacha Yawe na kuitumikia miungu mingine. 17Maana, Yawe, Mungu wetu, ndiye aliyetutoa sisi pamoja na wazee wetu katika inchi ya Misri tulikokuwa watumwa, tukayaona kwa macho yetu wenyewe matendo ya ajabu aliyotenda. Akatulinda katika safari zetu zote na kati ya watu wote ambao tulipita kati yao.
18“Yawe alituondolea watu wote, ni kusema Waamori wote waliokaa katika inchi. Kwa hiyo, nasi tutamutumikia Yawe, maana ndiye Mungu wetu.”
19Lakini Yoshua akawaambia: “Ninyi hamuwezi kumutumikia Yawe, maana yeye ni Mungu Mutakatifu. Yeye ni Mungu mwenye wivu, naye hatawasamehe makosa na zambi zenu. 20Mukimwacha Yawe na kuitumikia miungu ya kigeni, atawaazibu na kuwaangamiza ninyi, hata ingawa amewatendea mema haya yote.” 21Nao watu wakamwambia Yoshua: “Hapana! Sisi tutamutumikia Yawe tu.” 22Halafu Yoshua akawaambia: “Ninyi ni washuhuda wenu wenyewe kwamba mumechagua kumutumikia Yawe.” Nao wakamujibu: “Sisi ni washuhuda.” 23Naye akawaambia: “Basi, muondoe miungu ya kigeni munayokuwa nayo, mumufuate Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wenu wote.” 24Nao, wakasema: “Tutamutumikia na kumutii Yawe, Mungu wetu.” 25Hivyo, Yoshua akafanya agano na Waisraeli kule Sekemu, akawapa masharti na maagizo ya kufuata. 26Yoshua akayaandika haya yote katika kitabu cha sheria ya Mungu; kisha, akatwaa jiwe kubwa na kulisimika chini ya muti wa mwalo katika hema ya Yawe. 27Halafu akawaambia watu wote: “Jiwe hili ndilo litakalokuwa ushuhuda kwetu, maana limesikia maneno yote ambayo Yawe ametuambia. Kwa hiyo, litashuhudia juu yenu, kusudi musipate kumwasi Mungu wenu.” 28Halafu Yoshua akawaruhusu watu waondoke; nao wakaenda kila mumoja kwake.
Kifo cha Yoshua
29Nyuma ya mambo hayo, Yoshua mwana wa Nuni na mutumishi wa Yawe, akakufa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi. 30Nao wakamuzika kwenye eneo ambalo alikuwa amegawanyiwa kuwa sehemu yake, kule Timunati-Sera, katika milima ya Efuraimu, upande wa kaskazini wa mulima wa Gasi.
31Waisraeli walimutumikia Yawe muda wote wa maisha ya Yoshua, na nyuma ya kifo chake, waliendelea kumutumikia kwa muda wa maisha ya wale wazee waliokuwa wameona kwa macho yao mambo yale Yawe aliyowatendea Waisraeli.
32Mifupa ya Yosefu ambayo Waisraeli walikuwa wameileta kutoka Misri waliizika kule Sekemu katika eneo ambalo Yakobo alikuwa amelinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba ya Sekemu, kwa bei ya vikoroti mia moja vya feza. Eneo lile nalo likakuwa mali yao wazao wa Yosefu.
33Naye Eleazari mwana wa Haruni, akakufa na kuzikwa Gibea, muji ambao mwana wake Finehasi alikuwa amepewa katika inchi ya milima ya Efuraimu.

Currently Selected:

Yoshua 24: SWC02

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in