Yeremia UTANGULIZI
UTANGULIZI
Nabii Yeremia aliishi na kufanya kazi yake mpaka miaka michache mbele ya watu wa Yuda kupelekwa katika uhamisho, katika mwaka 586 mbele ya Kristo. Yeremia alizaliwa katika jamaa ya makuhani, akaitwa na Mungu akiwa bado kijana kusudi akuwe musemaji wake. Alikuwa mutu mutulivu ambaye alipambana na wafalme, makuhani, manabii wengine wa uongo na hata taifa lote la Israeli.
Sehemu hizi zinaweza kutambuliwa katika kitabu hiki:
Sura 1-25. Katika sehemu hii kuna habari nyingi juu ya Yeremia mwenyewe; mwito wake, kazi yake kama nabii, na mambo yaliyomutokea katika nyakati za mufalme Yosia, mufalme Yoakini na mufalme Zedekia.
Sura 26-45. Sehemu hii inaelekea mambo Yeremia aliyosema na kufanya miaka ya mwishomwisho mbele ya utawala wa Yuda kuangushwa.
Sura 46-51. Kama vile katika kitabu cha Isaya, vilevile na katika Yeremia, kuna mukusanyiko wa makaripio na maonyo juu ya mataifa mengine: Misri, Filistia, Moabu, Amoni, Edomu, Damasiki, Arabia, Elamu na Babeli.
Sura 52. Kitabu kinaishia na habari ya historia–mambo yaliyotokea juu ya kutekwa kwa Yerusalema na watu kupelekwa katika uhamisho Babeli, inchi ya Wakaldea (angalia 2 Wafalme 24.18–25.30).
Currently Selected:
Yeremia UTANGULIZI: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.