YouVersion Logo
Search Icon

Isaya 8

8
Teka haraka, nyanganya upesi
1Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”#8.1 Teka-haraka-nyanganya-upesi: Kiebrania: Maher-shalal-hash-bazi. 2Basi, nikajipatia washuhuda wawili waaminifu ambao wangenishuhudia: Kuhani Uria na Zekaria mwana wa Yeberekia. 3Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.” 4Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.
Mufalme wa Asuria anakuja
5Yawe alisema nami tena, akaniambia: 6Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia, 7basi, Bwana wao atawaletea mafuriko makubwa ya maji ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria na nguvu zake zote; yatafurika na kupita kingo zake. 8Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!
Mipango ya bure ya watu
9Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa!
Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia!
Mujiweke tayari na kufezeheshwa.
Mujiweke tayari na kufezeheshwa.
10Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure;
mufanye mipango lakini haitawezekana,
maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.
Maonyo kwa nabii
11Yawe alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia: 12Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu. #Ang. 1 Pet 3.14-15 13Munitambue mimi peke yangu, Yawe wa majeshi, kuwa mutakatifu. Muniogope na kuniabudu mimi peke yangu. 14Mimi nitakuwa kimbilio. Nitakuwa vilevile kama jiwe la kujikwaa, jiwe kubwa la kuziangusha falme za Israeli na Yuda. Nitakuwa mutego wa kuwatega na kuwanasa wakaaji wa Yerusalema. #Ang. 1 Pet 2.8 15Watu wengi watajikwaa, wataanguka na kupondekana; watanaswa katika mutego huo na kukamatwa mateka.
Maonyo juu ya kushauriana na mizimu
16Nitalinda agizo hilo na kuchunga mafundisho hayo kati ya wafuasi wangu. 17Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia. #Ang. Ebr 2.13 18Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni. #Ang. Ebr 2.13
19Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima. 20Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.
Taabu
21Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni 22na kuiangalia dunia, lakini wataona tu taabu, giza na mateso makubwa. Hakuna atakayeepuka giza hilo kubwa.
Mutoto amezaliwa kwetu
23Lakini inchi ile iliyokuwa imepatwa na huzuni haitabaki siku zote katika giza hilo kubwa. Hapo zamani Mungu alizifezehesha inchi za Zebuluni na Nafutali, lakini siku zinazokuja atafanya kuwa na utukufu kandokando ya bahari, inchi inayokuwa ngambo ya Yordani, na hata Galilaya ambamo watu wa mataifa wanaishi. #Ang. Mat 4.15

Currently Selected:

Isaya 8: SWC02

Highlight

Copy

Compare

Share

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in