Hagai 2
2
Uzuri wa hekalu jipya
Watu wanatii amri ya Yawe
1Katika siku makumi mbili na moja, mwezi wa saba mwaka uleule, neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Hagai na kusema hivi: 2Sema na mutawala wa Yuda, Zerubabeli mwana wa Saltieli, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki na watu waliorudi kutoka katika uhamisho uwaambie hivi: 3Ni nani kati yenu anayekumbuka jinsi nyumba hii ilivyokuwa yenye utukufu? Sasa munaiona namna gani? Bila shaka sasa munaiona kama si kitu. #Ang. Ezra 3.12 4Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii.
–Ni ujumbe wa Yawe!
Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
5Mulipotoka Misri niliwaahidi kwamba nitakuwa pamoja nanyi siku zote. Basi, ningali pamoja nanyi, kwa hiyo, musiogope kitu. #Ang. Kut 29.45-46
6Yawe wa majeshi anasema hivi: Kisha muda kidogo nitazitikisa mbingu na dunia, bahari na inchi kavu. #Ang. Ebr 12.26 7Nitayatikisa mataifa yote na mali zao zote zitaletwa humu, nami nitaifanya nyumba hii kuwa yenye utukufu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.
8Feza na zahabu yote katika dunia ni mali yangu.
–Ni ujumbe wa Yawe.
9Nyumba mupya itakuwa yenye utukufu zaidi kuliko ile ya kwanza.
–Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo!
Kutoka hapa nitawapa watu wangu fanaka.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Watu wote ni wachafu
10Katika siku ya makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, katika mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe wa majeshi lilimufikia nabii Hagai kusema hivi: 11Yawe wa majeshi anasema hivi: Makuhani watoe uamuzi juu ya jambo hili: 12Kama mutu akibeba kipande cha nyama iliyotakaswa katika upindo wa nguo yake, kisha akigusa kwa upindo wa nguo ile mukate au chakula kilichopikwa, au divai, au mafuta au chakula cha aina yoyote ile, basi, chakula hicho kitakuwa kitakatifu?
Makuhani wakamujibu: Hapana.
13Hagai akawauliza tena: Mutu anayehesabiwa kuwa muchafu kwa kugusa maiti, akigusa sehemu ya vyakula hivi, chakula hicho kitakuwa kichafu?
Makuhani wakamujibu: Ndiyo, kitakuwa kichafu. #Ang. Hes 19.11-22
14Hagai akajibu na kusema hivi: Hivi ndivyo inavyokuwa kwa watu wa taifa hili mbele yangu –ni ujumbe wa Yawe– na kila kitu wanachofanya; hata vitu wanavyotoa kwenye mazabahu ni vichafu.
15Lakini sasa mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Mbele ya kuanza kujenga upya nyumba yangu, 16hali yenu ilikuwa namna gani? Mutu alifika kwenye fungu la ngano akingojea kupata vipimo makumi mbili, lakini kulikuwa vipimo kumi tu. Mutu alifika kwenye mutungi wa divai akingojea kujaza vyombo makumi tano, lakini kulikuwa makumi mbili tu. 17Mimea yenu yote muliyojaribu kupanda, niliiharibu kwa kuikausha na kwa kuipiga kwa ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
18Sasa, mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Leo ni siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, siku ambayo musingi wa hekalu umekamilika. Basi mufikiri vizuri: 19Ingawa sasa hakuna ngano ndani ya gala, nayo mizabibu, tini, mikomamanga na mizeituni haijazaa kitu, lakini tangu leo, nitawabariki.
Ahadi kwa Zerubabeli
20Siku ileile ya makumi mbili na ine, mwezi wa kenda, neno la Yawe lilimufikia Hagai kwa mara ya pili kusema hivi: 21Sema na Zerubabeli mutawala wa Yuda umwambie hivi: Nitazitikisa mbingu na dunia 22na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao. 23Siku hiyo, nitakutwaa wewe Zerubabeli mwana wa Saltieli, mutumishi wangu.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Nitakusimika utawale kwa jina langu.
–Ni ujumbe wa Yawe!
Wewe ndiwe niliyekuchagua.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Currently Selected:
Hagai 2: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.