YouVersion Logo
Search Icon

Mwanzo 3

3
Uasi wa mwanadamu
1Nyoka alikuwa mwerevu kuliko nyama wote wa pori walioumbwa na Yawe Mungu. Basi, nyoka akamwambia yule mwanamuke: “Ni kweli Mungu alisema musikule matunda ya muti wowote katika bustani?”
2Mwanamuke akamujibu yule nyoka: “Tunaweza kula matunda ya miti katika bustani 3lakini Mungu alisema: ‘Musikule matunda ya muti unaokuwa katikati ya bustani, wala musiuguse. Kama sivyo, mutakufa.’ ”
4Nyoka akamwambia mwanamuke: “Hamutakufa! 5Mungu alisema hivyo kwa sababu anajua kwamba mukikula matunda ya muti ule mutafumbuliwa macho, nanyi mutakuwa kama Mungu, mukijua mazuri na mabaya.”
6Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula. 7Mara moja macho yao yakafumbuliwa, wakatambua kwamba wako uchi. Kwa hiyo wakashona majani ya muti wa tini, wakajifanyia nguo.
8Magaribi mwanaume na muke wake wakasikia Yawe Mungu akitembea katika bustani, nao wakajificha kati ya miti ya bustani, Yawe Mungu asipate kuwaona. 9Lakini Yawe Mungu akamwita yule mwanaume: “Uko wapi?”
10Naye akamujibu: “Nilisikia sauti yako katika bustani, nikaogopa maana nilikuwa uchi. Nikajificha.”
11Yawe akamwuliza: “Nani aliyekuambia kwamba uko uchi? Umekula tunda la muti nililokuamuru usikule?”
12Yule mwanaume akajibu: “Mwanamuke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la muti ule, nami nikakula.”
13Yawe Mungu akamwuliza yule mwanamuke: “Umefanya nini wewe?”
Mwanamuke akamujibu: “Nyoka alinidanganya, nami nikakula.”
Azabu
14Kisha Yawe akamwambia nyoka:
“Kwa sababu umefanya hivyo,
umelaaniwa kuliko nyama wote wa kufugwa,
na kuliko nyama wote wa pori.
Utatambaa kwa tumbo lako
na kula mavumbi siku zote za maisha yako.
15Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke,
kati ya uzao wako na uzao wake.
Yeye ataponda kichwa chako,
nawe utamwuma kisigino chake.”
16Kisha akamwambia mwanamuke:
“Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa,
Utazaa watoto kwa uchungu.
Utakuwa na hamu na mume wako,
naye atakutawala.”
17Kisha akamwambia yule mwanaume:
“Wewe umemusikiliza muke wako
na kula matunda ya muti ambayo nilikuamuru usikule.
Basi, udongo umelaaniwa kwa sababu yako.
Kwa jasho utajipatia toka humo chakula chako,
siku zote za maisha yako.
18Udongo utakuzalia miiba na magugu,
nawe utakula majani ya shamba.
19Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula,
mpaka utakaporudi katika udongo,
maana ulitwaliwa katika udongo.
Wewe ni mavumbi
na utarudi katika mavumbi.”
20Adamu#3.20 Adamu: Kiebrania maana yake ni “mutu”. akamupa muke wake jina “Eva”,#3.20 Eva: Kiebrania kinalingana na neno lenye maana “uzima”. maana alikuwa mama wa wanadamu wote. 21Yawe Mungu akawatengenezea Adamu na muke wake nguo za ngozi, akawavalisha.
Adamu na Eva wanafukuzwa katika bustani
22Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.” 23Basi, Yawe Mungu akamufukuza Adamu inje ya bustani ya Edeni, kusudi alime udongo ambamo alitwaliwa. 24Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.

Currently Selected:

Mwanzo 3: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy