YouVersion Logo
Search Icon

Ezekieli 45

45
Sehemu ya inchi takatifu kandokando ya hekalu
1Mutakapoigawanya inchi kwa kupiga kura kusudi kila kabila lipate sehemu yake, sehemu moja ya inchi ni lazima itakaswe kwa ajili ya Yawe. Urefu wake utakuwa kilometre kumi na mbili na nusu na upana kilometre kumi. Eneo hilo lote litakuwa takatifu. 2Ndani yake kutakuwa eneo muraba kwa ajili ya patakatifu, kila upande metre mia mbili makumi tano, na litazungukwa na eneo wazi lenye upana wa metre mia mbili makumi tano. 3Katika eneo hilo utapima vilevile sehemu yenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre tano; humo kutakuwa hekalu langu, Pahali Patakatifu Sana. 4Eneo hilo litakuwa takatifu katika inchi, na kutengwa kwa ajili ya makuhani wanaomutumikia Yawe katika hekalu lake. Ndani ya eneo hilo kutakuwa nyumba zao na nafasi iliyotakaswa kwa ajili ya hekalu langu. 5Eneo lingine lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre tano, litatengwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika katika hekalu likuwe urizi wao.
6Mutapima eneo la muji karibu na eneo takatifu, lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre mbili na nusu. Hilo litakuwa kwa ajili ya mutu yeyote wa Israeli.
Sehemu ya ufalme wa Waisraeli
7Mukubwa, naye atapewa eneo lake upande wa mashariki na magaribi wa eneo lililotakaswa kwa ajili ya Yawe. Eneo hilo litaenea tangia upande wa magaribi mpaka kwenye bahari ya Mediteranea na upande wa mashariki mpaka upande wa mashariki wa inchi. Litakuwa na urefu sawa na eneo lililopewa kwa kila kabila la Waisraeli. 8Huo ndio urizi wa mufalme katika Israeli. Hivyo mufalme hatawatesa watu wangu, lakini ataacha inchi igawanywe kwa Waisraeli kulingana na makabila ya Israeli.
Mapaswa ya mufalme
9Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi wakubwa wa Waisraeli, mumefanya zambi vyakutosha. Muache kutesa watu kwa ukali. Muimarishe sheria yangu na haki. Muache kuwafukuza watu wangu katika inchi.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
10Kila mutu anapaswa kutumia mizani na vipimo vya haki. #Ang. Law 19.36 11Kwa kipimo cha ulinganifu: efa kwa unga na bati kwa mafuta zina kipimo sawasawa. Hivyo viwili ni sehemu moja ya kumi ya homeri moja.#45.11 homeri: chombo cha kupimia vitu vyenye kukauka au vya majimaji kama litre 175; hivyo efa au bati ingekuwa na litre 17.5. 12Kwa kupima uzito: gera makumi mbili ni shekeli#45.12 Shekeli: wakati wa Ezekieli labda ilikuwa na uzito wa kilo 11.4. moja, shekeli makumi tano ni mina moja.
13Vipimo vya matoleo yenu ya vyakula vitakuwa hivi: sehemu moja ya sita ya efa katika homeri moja ya ngano, na moja ya sita ya efa katika homeri moja ya shayiri. 14Kiwango cha mafuta kitakuwa hivi: sehemu moja ya bati ya mafuta kutoka kila kori (kori moja ni sawa na homeri moja ambayo ni sawa na bati kumi). 15Watatoa kondoo mumoja kwa kila kundi la kondoo mia mbili katika jamaa za Waisraeli. Wataleta sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani, kusudi wapate kufanyiwa upatanisho. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– 16Watu wote wa inchi watamupatia mufalme wa Waisraeli sadaka hizo. 17Itakuwa ni mapaswa ya mufalme kuhakikisha kuwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za vyakula na sadaka za kinywaji zinazotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi, Sabato, na sikukuu zozote zilizowekwa kwa Waisraeli, zinapatikana. Mufalme yeye mwenyewe atatayarisha sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani kwa kuwafanyia watu wote wa Israeli upatanisho.
Sikukuu
(Kut 12.1-20; Law 23.33-43)
18Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mutatoa sadaka ya mwana-ngombe dume asiyekuwa na kilema kwa kutakasa hekalu langu. 19Kuhani atatwaa sehemu ya damu ya sadaka ya kusamehewa zambi na kuipaka kwenye miimo ya nyumba ya Yawe, pembe za mazabahu, na miimo ya nafasi ya kuingilia kwenye kiwanja cha ndani. 20Atafanya vile vile siku ya saba ya mwezi huo, kwa ajili ya kila mutu aliyetenda zambi bila kukusudia au kwa kutokujua. Kwa njia hiyo mutaitakasa nyumba ya Yawe.
21Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mutafanya sikukuu ya Pasaka. Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. #Ang. Kut 12.1-20; Hes 28.16-25 22Siku hiyo, mufalme atatoa ngombe dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya kusamehewa zambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa Israeli. 23Kila siku, katika muda huo wa siku saba, atamutolea Yawe sadaka ya ngombe dume saba na kondoo dume saba wasiokuwa na kilema kwa kuwateketeza kwa moto. Tena ni lazima atoe sadaka kila siku kuwa sadaka ya kusamehewa zambi. 24Kisha atatengeneza sadaka ya unga kilo kumi kwa kila ngombe dume na kilo kumi kwa kila kondoo dume, halafu litre tatu za mafuta kwa kila kilo kumi za unga.
25Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, na kwa muda wa siku saba za sikukuu, mufalme atatoa mahitaji kwa ajili ya sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za kuteketezwa kwa moto, sadaka za vyakula na mafuta. #Ang. Law 23.33-36; Hes 29.12-38

Currently Selected:

Ezekieli 45: SWC02

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in