YouVersion Logo
Search Icon

Ezekieli 31

31
Misri inalinganishwa na muti wa mwerezi
1Katika siku ya kwanza ya mwezi wa tatu, mwaka wa kumi na mumoja tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: 2Wewe mwanadamu! Umwambie Mufalme wa Misri na watu wake wote hivi:
Wewe unafanana na nini kwa ukubwa wako?
3Wewe ni kama muti wa mwerezi wa Lebanoni
wenye matawi mazuri na majani mengi na shina refu.
Kilele chake kinafika hata katika mawingu.
4Maji yaliustawisha,
vilindi vya maji viliulisha.
Mito ilibubujika pahali ulipoota,
ikapeleka vijito kwenye miti yote ya pori.
5Kwa hiyo, ulirefuka sana
kupita miti yote katika pori;
matawi yake yalizidi kuwa mengi na makubwa,
kutokana na maji mengi ndani ya mizizi yake.
6Ndege wote waliweka chicha katika matawi yake,
nyama wa pori walizalia chini yake,
mataifa yote makubwa yalikaa chini ya kivuli chake.
7Ulikuwa muzuri kwa ukubwa wake,
na kwa urefu wa matawi yake.
Mizizi yake ilipenya chini
mpaka penye maji mengi.
8Kati ya miti ya mierezi ya bustani ya Mungu,
hakuna muti uliolingana nao,
wala misunobari haikulingana na matawi yake,
mibambakofi haikuwa na matawi kama yake,
hata muti wowote wa bustani ya Mungu
haukulingana nao kwa uzuri. #Ang. Mwa 2.9
9Mimi niliufanya kuwa muzuri
kwa matawi yake mengi;
ulionewa wivu na miti yote ya Edeni
iliyokuwa katika bustani ya Mungu.
10Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu ulirefusha kimo chake na kufikisha kilele chake katika mawingu makubwa, ukajivunia urefu wake, 11nitautia katika mikono ya mukubwa kati ya mataifa. Yeye, atauazibu. Nimeutupilia mbali kadiri ya uovu wake. 12Watu wa mataifa mengine ya hatari sana, wataukata na kuuangusha chini na kuulalisha chini. Matawi yake yataanguka chini kwenye mulima na kila pahali katika mabonde; yatavunjika na kulala chini katika mitelemuko yote. Watu wote wataondoka chini ya kivuli chake na kuuacha. 13Ndege wote watatua juu ya mabaki yake na nyama wote wa pori watakanyaga matawi yake. 14Hayo yameupata kusudi muti wowote unaokuwa pahali penye maji usiweze kurefuka tena kwa kimo hicho wala kukifikisha kilele chake katika mawingu. Muti wowote unaokunyweshwa maji usiweze tena kufikia urefu huo. Kwa maana kila kitu mwisho wake ni kifo; hata na watu vilevile. Wote watashiriki hali ya wanaoshuka katika shimo kwa wafu.
15Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ileile muti wa mwerezi ulipofika katika kuzimu nilitandaza giza nene juu yake, nikaufunika; mito yake niliikausha na mutiririko wa maji yake mengi nikaukomesha. Nayo Lebanoni niliiweka katika giza kwa ajili yake, na miti yote katika pori ikazimia kwa ajili yake. 16Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa sauti ya kuanguka kwake, wakati nilipouangusha chini katika kuzimu pamoja na wale wanaoshuka ndani ya shimo kwa wafu. Nayo miti yote ya Edeni, miti mizuri na ya pekee ya Lebanoni ambayo ilimwangiliwa maji, ilifarijiwa huko chini kwa wafu. 17Hiyo nayo ilishuka kule katika kuzimu pamoja nao, ikajiunga na wale waliofungamana nao na ambao waliikaa chini ya kivuli chake.
18Kwa uzuri na ukubwa wa muti huo, hakuna muti wowote katika bustani ya Edeni ambao uliweza kulinganishwa nao. Sasa, muti huo ni wewe Mufalme wa Misri. Wewe utatupwa chini kwa wafu pamoja na miti ya Edeni. Utalala karibu na wale wasiomujua Mungu na wale waliouawa kwa upanga. Hiyo itakuwa hali yako ewe Mufalme wa Misri, wewe na watu wako.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

Currently Selected:

Ezekieli 31: SWC02

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in