Ezekieli 26
26
Unabii juu ya Tiro
1Katika siku ya kwanza ya mwezi, mwaka wa kumi na mumoja tangia kuhamishwa kwetu, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: #Ang. Isa 23.1-18; Yoe 3.4-8; Amo 1.9-10; Zak 9.1-4; Mat 11.21-22; Lk 10.13-14 2Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika! 3Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitapingana nawe ewe Tiro. Nitasukuma mataifa mengi juu yako, nao watakuja kama mawimbi ya bahari. 4Wataziharibu kuta zako na kuibomoa minara yako. Nitafagia kabisa udongo wako na kukufanya kuwa kama jiwe tupu. 5Utakuwa pahali penye kukauka katikati ya bahari, na wavuvi watakaushia nyavu zao hapo.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Mataifa yatakukamata mateka, 6na miji inayokuwa jirani yako huko katika vijiji itaangamizwa. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.
7Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kutoka upande wa kaskazini nitamuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mufalme wa wafalme, akiwa na farasi, magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa, akuje kukushambulia. 8Ataiangamiza miji inayokuwa jirani yako huko katika vijiji. Kisha atajenga kuta za kukushambulia, atajaza udongo kwenye kuta zako na kuweka ukuta wenye ngao kwa kukushambulia. 9Ataweka vifaa vyake vya kubomoa mbele ya kuta zako, na kwa nyundo ataivunjavunja minara yako. 10Farasi wa mufalme Nebukadneza ni wengi na mavumbi watakayorusha juu yatakufunika. Kuta zako zitatetemeka kwa mushindo wa waaskari wapanda-farasi na magari ya vita na ya mizigo wakati atakapoingia kwenye milango yako kama watu wanavyoingia katika muji kupitia pahali palipobomolewa. 11Kwa kwato za farasi wake, atakanyagakanyaga barabara zako zote. Atawaua watu wako kwa upanga; minara yako mikubwa ataiangusha chini. 12Ataunyanganya utajiri wako pamoja na biashara yako. Atazibomoa kuta zako na kuziangusha nyumba zako nzuri; mawe, mbao na udongo ulivyotumia kwa kujenga nyumba hizo watavitupa katika bahari. 13Nitakomesha muziki wa nyimbo zako. Sauti za vinubi vyako hazitasikilika tena. 14Nitakufanya kuwa kama jiwe; utakuwa pahali pa wavuvi pa kukaushia nyavu zao, wala hautajengwa tena. Mimi Yawe nimesema.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
15Bwana wetu Yawe anasema hivi kwa Tiro: Wakaaji wa sehemu za kandokando ya bahari watatetemeka watakaposikia kishindo cha kuanguka kwako na mulio wa maumivu na wa watu wanaouawa. 16Wakubwa wote wa mataifa ya kandokando ya bahari watashuka toka kwenye viti vyao vya kifalme, na kuvua nguo zao za heshima pamoja na nguo zao zilizopindwa. Kisha kujaa hofu, wataikaa chini; nao watatetemeka wakati wote na kushangaa sana juu ya hayo yaliyokupata. #Ang. Ufu 18.9-10 17Watakuimbia wimbo huu wa kuomboleza:
Namna gani wewe muji wenye utukufu,
umetoweka kutoka katika bahari!
Ulikuwa na nguvu juu ya bahari,
wewe pamoja na wakaaji wako,
wewe uliyeletea woga juu ya wote!
18Sasa watu wa visanga wanatetemeka
kwa sababu ya kuanguka kwako;
watu wa visanga katika bahari wanatishwa
kwa kuanguka kwako!
19Maana, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakufanya wewe Tiro kuwa matongo, kama miji isiyokuwa na watu, nitakapoleta juu yako maji kutoka vilindi vya bahari, na maji mengi yatakufunika. 20Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima. 21Nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha na itakuwa mwisho wako; watu watakutafuta, lakini hawatakupata tena. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo. #Ang. Ufu 18.21
Currently Selected:
Ezekieli 26: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.