YouVersion Logo
Search Icon

Ezekieli 1:4-9

Ezekieli 1:4-9 SWC02

Nilipoangalia niliona upepo wa zoruba unavuma kutokea upande wa kaskazini: kulikuwa wingu kubwa lililozungukwa na mwangaza, na moto ulitokea humo mufululizo na katikati ya huo moto kulikuwa kitu kinachometameta kama shaba. Kutoka humo nilitambua viumbe vine, ambavyo vilionekana hivi: Vilikuwa na umbo la mwanadamu. Kila kimoja kilikuwa na nyuso ine na mabawa mane. Miguu yao ilikuwa yenye kunyooka; upande wa chini wa miguu yao ulikuwa kama kwato za miguu ya mwana-ngombe, nazo zilimetameta kama shaba safi. Chini ya mabawa yao, kulikuwa mikono inayokuwa sawa ya mutu. Mikono hiyo ilikuwa inaelekea kwenye pande zote ine pamoja na nyuso zao na mabawa yao. Incha za mabawa yao ziligusana kila bawa na bawa lingine. Vilipotembea, vilikwenda mbele moja kwa moja pasipo kugeuka.

Free Reading Plans and Devotionals related to Ezekieli 1:4-9