YouVersion Logo
Search Icon

Muhubiri UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu cha Muhubiri (Kiebrania: Koheleti) kina ujuzi wa mutu ambaye alifikiri sana juu ya ufupi wa maisha ya mwanadamu na mambo yake ya kutatiza, akachunguza na furaha yake, akaona hayo yote kuwa magumu yasiyoeleweka: “kila kitu ni bure”. Katika kule kuwaza na kuwaza kwake anaona kwamba haiwezekani kuelewa mipango ya Mungu ambaye anaongoza mambo katika dunia. Hata hivyo anawahimiza watu wafanye kazi kwa bidii na kufurahia vipaji walivyopewa na Mungu muda wote wanapoishi.
Mafikiri mengi ya Muhubiri huyu yanaonekana kuwa ya kutatiza na ya mashaka. Hata hivyo ana musimamo wa kidini na anatushauri kwa mwisho: “Umwogope Mungu, na ushike amri zake; kwa sababu hayo ndiyo madaraka ambayo mwanadamu aliumbwa kwa ajili yake.” (12.13)

Currently Selected:

Muhubiri UTANGULIZI: SWC02

Highlight

Copy

Compare

Share

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in