YouVersion Logo
Search Icon

2 Mambo ya Siku 36

36
Mufalme Yoahazi wa Yuda
(2 Fal 23.30-35)
1Watu wa inchi ya Yuda wakatwaa Yoahazi, mwana wa Yosia, wakamuweka kuwa mufalme pahali pa baba yake. 2Yoahazi alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitatu alipoanza kutawala; akatawala kwa muda wa miezi mitatu akiwa kule Yerusalema. 3Kisha mufalme wa Misri akamwondoa kule Yerusalema na kulipisha inchi kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu. 4Kisha mufalme wa Misri akamweka Eliakimu, ndugu ya Yoahazi kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema, na akabadilisha jina lake kuwa Yoyakimu; lakini Neko akamupeleka ndugu yake Yoahazi mpaka Misri.
Mufalme Yotakimu wa Yuda
(2 Fal 23.36–24.7) #Ang. Yer 22.11-12
5Yoyakimu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, akatawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Alitenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wake. #Ang. Yer 22.18-19; 26.1-6; 35.1-19 6Kisha Nebukadneza mufalme wa Babeli, akamushambulia, akamufunga kwa minyororo kwa kumupeleka Babeli. #Ang. Yer 25.1-38; 36.1-32; 45.1-5; Dan 1.1-2 7Nebukadneza akatwaa vilevile vyombo vimoja vya nyumba ya Yawe akavipeleka Babeli na kuviweka katika nyumba ya kifalme kule Babeli. 8Basi matendo mengine ya Yoyakimu, pamoja na machukizo aliyotenda na mambo mengine yaliyoonekana juu yake yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na Yuda; naye Yoyakini#36.8 Yoyakini: au: Yekonia. mwana wake akatawala pahali pake.
Mufalme Yoyakini wa Yuda
(2 Fal 24.8-17)
9Yoyakini alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala kule Yerusalema kwa muda wa miezi mitatu na siku kumi. Alitenda maovu mbele ya Yawe. 10Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema. #Ang. Yer 22.24-30; 24.1-10; 29.1-2; 37.1; Eze 17.12-13
Mufalme Sedekia wa Yuda
(2 Fal 24.18-20; Yer 52.1-3)
11Sedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala, akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka kumi na mumoja. #Ang. Yer 27.1-22; 28.1-17 12Alitenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wake, wala hakunyenyekea mbele ya nabii Yeremia ambaye alisema maneno yaliyotoka kwa Yawe.
Yerusalema inaangamia
(2 Fal 25.1-21; Yer 52.3-11)
13Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli. #Ang. Eze 17.15 14Hata makuhani, viongozi wa inchi ya Yuda pamoja na watu walikosa uaminifu kabisa wakiiga matendo yote ya kuchukiza ya watu wa mataifa mengine; waliichafua nyumba ya Yawe ambayo yeye mwenyewe alikuwa ameitakasa kule Yerusalema. 15Yawe, Mungu wa babu zao, mara kwa mara alituma kwao wajumbe wake maana alikuwa na huruma kwa watu wake na makao yake. 16Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha. 17Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake. #Ang. Yer 21.1-10; 34.1-5 18Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli. 19Aliichoma moto nyumba ya Mungu, akaubomoa ukuta wa Yerusalema, akazichoma moto nyumba zote za kifalme na kuharibu vyombo vyake vyote vya bei kali. 20Watu waliookolewa kwenye vita aliwapeleka katika uhamisho Babeli. Kule wakakuwa watumwa wake na wa wazao wake mpaka ufalme wa Persia ulipoinuka kwa nguvu. 21Na hivyo likatimia neno la Yawe alilosema kwa njia ya nabii Yeremia: “Mpaka inchi imetimiza Sabato zake#36.21 Pumziko la Sabato: Kwa kufuatana na Sheria, kila mwaka wa saba, inchi haikutakiwa ilimwe., haitalimwa siku zote itakapokuwa ukiwa mpaka miaka makumi saba itakapotimia.” #Ang. Yer 25.11; 29.10
Kiro anawaamuru Wayuda warudio kwao
(Ezra 1.1-4)
22Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, kusudi litimie neno la Yawe alilolisema kwa njia ya nabii Yeremia, Yawe aliamusha nia ya Kiro naye akatoa amri hii katika ufalme wake wote, vilevile alituma habari hizo kwa njia ya maandiko:
23“Hivi ndivyo anavyosema Kiro mufalme wa Persia: ‘Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote za ulimwengu, na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, katika inchi ya Yuda. Basi sasa kila mutu kati yenu, ninyi wote munaokuwa watu wa Yawe, Mungu wake akuwe pamoja naye, na aende.’ ” #Ang. Isa 44.28

Currently Selected:

2 Mambo ya Siku 36: SWC02

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in