2 Mambo ya Siku 10
10
Uasi wa makabila ya Kaskazini
(1 Fal 12.1-20)
1Basi, Rehoboamu akaenda Sekemu, ambako Waisraeli wote walikuwa wamekusanyika kwa kumuweka kuwa mufalme. 2Naye Yeroboamu mwana wa Nebati alipopata habari juu ya tendo hilo, wakati ule alikuwa angali anaishi Misri alikokwenda alipomukimbia Solomono, alirudi kutoka Misri. 3Lakini Waisraeli walituma ujumbe na kumwita. Kisha, yeye pamoja na Waisraeli wote walimwendea Rehoboamu na kumwambia: 4“Baba yako alitubebesha muzigo muzito. Basi, utupunguzie muzigo ule, nasi tutakutumikia.”
5Rehoboamu akawajibu: “Mwende murudie kwangu nyuma ya siku tatu.” Basi wakaondoka.
6Nyuma, Rehoboamu akataka kujua maoni ya wazee ambao walikuwa washauri wa baba yake Solomono alipokuwa angali muzima, akawauliza: “Munanishauria kwamba niwape jibu gani watu hawa?”
7Wazee wale wakamujibu: “Ukiwahurumia watu hawa, ukiwafurahisha na kusema nao maneno mazuri, pale watakuwa watumishi wako siku zote.”
8Lakini Rehoboamu alizarau shauri la wazee na kwa pahali pake akashauriana na vijana waliokomaa pamoja naye ambao walikuwa washauri wake. 9Basi, akawauliza: “Ninyi munatoa shauri gani kusudi tuweze kuwajibu watu hawa walioniambia: ‘Punguza muzigo ambao baba yako alitubebesha?’ ”
10Wale vijana wakamujibu: “Watu waliokuambia ‘Baba yako alitubebesha muzigo muzito, lakini wewe utupunguzie’, wewe uwaambie hivi: ‘Kidole changu kidogo cha mwisho ni kinene zaidi kuliko kiuno cha baba yangu. 11Muzigo wa baba yangu ulikuwa muzito, lakini wangu utakuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba.’ ”
12Basi katika siku ya tatu Yeroboamu pamoja na watu wote wakarudi kwa Rehoboamu kama vile alivyokuwa amewaagiza. 13Naye mufalme Rehoboamu akawajibu kwa ukali, akazarau shauri la wazee, 14na kufuata shauri la vijana wenzake. Basi akasema: “Baba yangu aliwabebesha muzigo muzito, lakini mimi nitaufanya kuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba” 15Halafu mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Mungu kusudi Yawe atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu, mwana wa Nebati kwa njia ya Ahiya wa Shilo.
16Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali walimwambia:
“Hatuna ushirika na Daudi!
Hatuna urizi kutoka kwa mwana wa Yese.
Kila mumoja arudie kwake,
enyi watu wa Israeli!
Utunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!”
Hivyo Waisraeli wote wakarudi kila mutu kwake. #Ang. 2 Sam 20.1 17Lakini Rehoboamu alitawala watu wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda. 18Kisha mufalme Rehoboamu akamutuma Hadoramu#10.18 Hadoramu: au: Adoniramu Ang. 1 Fal 4.6. aliyekuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa, nao watu wa Israeli walimupiga mawe, wakamwua. Halafu Rehoboamu akapanda ndani ya gari lake haraka akakimbilia Yerusalema. 19Hivyo, watu wa Israeli wakakuwa katika hali ya uasi juu ya utawala wa ukoo wa Daudi mpaka leo.
Currently Selected:
2 Mambo ya Siku 10: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.