1 Mambo ya Siku 9
9
Watu waliorudi toka katika utumwa
1Hivi, Waisraeli wote walihesabiwa kufuatana na vizazi vyao na kuandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli.
Watu wa Yuda wamepelekwa katika utumwa mpaka Babeli kwa sababu ya kutokuwa waaminifu. 2Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu. #Ang. Ezra 2.27; Neh 7.73 3Wamoja kati ya watu wa makabila ya Yuda, Benjamina, ya Efuraimu na Manase walikwenda kuishi Yerusalema:
4Katika kabila la Yuda, kulikuwa: Utai mwana wa Amihudi na mujukuu wa Omuri. Naye Omuri alikuwa baba ya Imuri na mujukuu wa Bani, wa wazao wa Peresi mwana wa Yuda. 5Asaya wa uzao wa Silo, aliyekuwa muzaliwa wa kwanza wa jamaa yake, pamoja na wana wake. 6Yeuli wa uzao wa Zera. Watu wa kabila la Yuda waliokaa Yerusalema walikuwa mia sita na makumi kenda kwa jumla.
7Katika kabila la Benjamina, kulikuwa: Salu mwana wa Mesulamu mwana wa Hodavia mwana wa Hasenua, 8Ibuneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Usi mwana wa Mikiri, Mesulamu mwana wa Sefatia mwana wa Rueli mwana wa Ibunia. 9Watu hao walikuwa wakubwa wa ukoo zao. Watu wa kabila la Benjamina watu waliokaa Yerusalema walikuwa mia kenda na makumi tano na sita.
Makuhani walioishi Yerusalema
10Hawa ndio makuhani walioishi Yerusalema: Yedaya, Yoyaribu na Yakini, 11Azariya mwana wa Hilkia mwana wa Mesulamu mwana wa Zadoki, mwana wa Merayoti mwana wa Ahitubu, aliyekuwa mukubwa wa nyumba ya Mungu; 12na Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pasuri mwana wa Malkia; na Masai mwana wa Adieli mwana wa Yazera mwana wa Mesulamu mwana wa Mesilemoti mwana wa Imeri.
13Wakubwa hawa wa ukoo za baba zao, pamoja na wandugu zao walikuwa kwa jumla watu elfu moja na mia saba na makumi sita. Walikuwa wakubwa wenye uwezo mukubwa katika kazi yote ya nyumba ya Mungu.
Walawi walioishi Yerusalema
14Hawa ndio Walawi walioishi Yerusalema: Semaya, mwana wa Hasubu mwana wa Azirikamu mwana wa Hasabia, wa ukoo wa Merari; 15na Bakibakari, na Heresi, na Galali, Matania mwana wa Mika mwana wa Sikiri mwana wa Asafu; 16na Obadia mwana wa Semaya mwana wa Galali mwana wa Yedutuni; na Berekia mwana wa Asa mwana wa Elekana; waliokuwa wakiishi katika vijiji vya Wanetofati.
Walinzi wa hekalu waliokuwa wakiishi Yerusalema
17Hawa ndio walinzi wa hekalu walioishi katika Yerusalema: Salumu, Akubu, Talmoni na Ahimani na wandugu zao. Salumu alikuwa mukubwa wao. 18Hata kufikia wakati ule, walinzi kutoka katika ukoo zao ndio waliolinda mulango wa mufalme#9.18 Mulango wa mufalme: mulango wa upande wa mashariki aliopitia mufalme. wa upande wa mashariki. Zamani, walikuwa walinzi wa viingilio vya makambi ya Walawi.
19Salumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu, pamoja na wandugu zake wa ukoo wa Kora, walikuwa na kazi ya kutunza viingilio vya hema la mukutano, kama vile babu zake walivyokuwa wakati wa ulinzi wa kambi ya Yawe. 20Finehasi mwana wa Eleazari, alikuwa musimamizi wao, zamani, Yawe alikuwa pamoja naye. 21Zekaria mwana wa Meselemia, alikuwa vilevile mulinzi wa viingilio vya hema la mukutano.
22Kwa jumla, watu mia mbili na kumi na wawili walichaguliwa kuwa walinzi wa viingilio vya hekalu. Waliandikwa kulingana na vijiji walimoishi. Mufalme Daudi na nabii Samweli ndio waliowaweka kwa kazi zao kwa sababu ya uaminifu wao. 23Basi, watu hao na wazao wao, waliendelea kulinda milango ya nyumba ya Yawe.
24Kila upande, ni kusema mashariki, magaribi, kaskazini na kusini, kulikuwa mulango uliokuwa na walinzi. 25Walinzi hawa walisaidiwa na wandugu zao waliokuwa wakiishi katika vijiji, ambao walilazimishwa kushika zamu ya ulinzi kwa muda wa siku saba, mara kwa mara, 26kwa maana wale walinzi wakubwa wane, ambao walikuwa Walawi, walikuwa na kazi ya kusimamia vyumba na hazina ya nyumba ya Mungu. 27Wao waliishi karibu na nyumba ya Mungu kwa sababu ilikuwa ni kazi yao kulinda na kufungua milango yake kila siku asubui.
28Walawi wengine walisimamia vyombo vilivyotumika wakati wa ibada. Walihitajika kuvihesabu wakati vilipotolewa na wakati viliporudishwa. 29Wengine walichaguliwa kusimamia vifaa vya hekalu, na vyombo vyote vitakatifu, na unga safi, divai, mafuta ya mizeituni, ubani na marasi. 30Lakini kazi ya kuchanga marasi ilifanywa na makuhani.
31Metitia, mumoja wa Walawi aliyekuwa muzaliwa wa kwanza wa Salumu, wa ukoo wa Kora, alisimamia utengenezaji wa sadaka ya mikate nyembamba. 32Nao wandugu zao wengine wa ukoo wa Kohati walikuwa na kazi ya kutayarisha mikate iliyotolewa kwa Mungu kila siku ya Sabato.
33Jamaa zingine za Walawi zilisimamia kazi ya nyimbo katika hekalu. Waliishi katika vyumba vimoja vya majengo ya nyumba ya Mungu na hawakuhitajika kufanya kazi ingine yoyote kwa maana walikuwa wakitumika usiku na muchana.
Babu na wazao wa mufalme Saulo
(8.29-38)
34Watu wote hawa waliotajwa walikuwa viongozi wa kabila la Walawi, kulingana na ukoo zao. Wao ndio viongozi walioishi Yerusalema.
35Yeieli alikuwa babu ya wakaaji wa muji wa Gibeoni ambamo aliishi yeye pamoja na muke wake aliyeitwa Maka. 36Muzaliwa wake wa kwanza aliitwa Abudoni, naye alifuatiwa na Zuri, Kisi, Bali, Neri, Nadabu, 37Gedori, Ahio, Zekaria na Mikloti. 38Mikiloti alizaa Simeamu. Wazao wao waliishi Yerusalema karibu na jamaa zingine za ukoo zao.
39Neri alizaa Kisi, naye Kisi alizaa Saulo. Saulo alikuwa na wana wane: Yonatani, Malikisua, Abinadabu na Esibali. 40Yonatani alizaa Meribu-Bali, Meribu-Bali alizaa Mika. 41Mika alikuwa na wana wane: Pitoni, Meleki, Tarea na Ahazi. 42Ahazi alizaa Yara, Yara alizaa Alemeti, Azimaweti na Zimuri, naye Zimuri alizaa Moza, 43Moza alizaa Binea, Binea alizaa Refaya, Refaya alizaa Eleasa, naye Eleasa alizaa Aseli.
44Aseli alikuwa na wana sita: Azirikamu, Bokeru, Isimaeli, Searia, Obadia na Hamani. Hawa wote walikuwa wana wa Aseli.
Currently Selected:
1 Mambo ya Siku 9: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.