YouVersion Logo
Search Icon

1 Mambo ya Siku 20

20
Daudi ananyanganya muji wa Raba
(2 Sam 12.26-31)
1Ilipokuwa wakati wa kipwa, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Yoabu akaongoza jeshi na kuharibu inchi ya Waamoni, akaenda vilevile na kuzunguka muji wa Raba kwa vita. Lakini Daudi alibaki kule Yerusalema. Naye Yoabu akashambulia muji wa Raba na kuuteka. #Ang. 2 Sam 11.1 2Kisha Daudi akatwaa taji ya mufalme wao kutoka juu ya kichwa chake, naye akagundua kwamba taji hiyo ilikuwa na uzito wa kilo makumi tatu na tano za zahabu na ndani yake mulikuwa jiwe la bei kali. Daudi akavikwa taji hiyo juu ya kichwa chake. Vilevile alinyanganya vitu vingi sana kutoka katika muji ule. 3Halafu akakamata watu wa muji ule, nao wakafanya kazi wakitumia misumeno, sururu za chuma na mashoka ya chuma. Ni vile ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote wakarudi Yerusalema.
Vita na majitu ya Wafilistini
(2 Sam 21.15-22)
4Nyuma ya hayo, kukatokea vita na Wafilistini kule Gezeri. Sibekayi wa muji wa Husati akamwua Sipayi aliyekuwa mumoja kati ya wazao wa majitu;#20.4 wazao wa majitu: Kiebrania: Warefai. hivyo Wafilistini wakashindwa.
5Kukatokea tena vita na Wafilistini. Naye Elihanani mwana wa Yairi akamwua Lami ndugu ya Goliati wa muji wa Gati ambaye mupini wa mukuki wake ulikuwa kama muti wa mufumaji wa nguo. #Ang. 1 Sam 17.4-7
6Nyuma kukatokea tena vita kule Gati ambako kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa murefu sana, na vidole sita katika kila mukono, na vidole sita katika kila muguu, kwa jumla vidole makumi mbili na vine. Yeye vilevile alikuwa wa uzao wa majitu. 7Naye alipowatukana Waisraeli, Yonatani mwana wa Simea, ndugu ya Daudi, akamwua.
8Hao walikuwa wazao wa majitu kule Gati, nao wakauawa na Daudi pamoja na watumishi wake.

Currently Selected:

1 Mambo ya Siku 20: SWC02

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in