1 Mambo ya Siku 13
13
Sanduku la Agano linasimamishwa Kiriati-Yearimu
(2 Sam 6.1-11)
1Daudi akashauriana na majemadari wa makundi ya maelfu na makundi ya mamia, pamoja na viongozi wote. 2Kisha akawaambia Waisraeli wote waliokusanyika: “Ikiwa mutakubaliana nami, na ikiwa ni mapenzi ya Yawe, Mungu wetu, tufanye hivi: tutume wajumbe waende wawaite wandugu zetu waliobaki katika inchi ya Israeli, pamoja na makuhani na Walawi wanaokuwa katika miji yao na mashamba ya malisho yao, wakuje kukusanyika pamoja nasi. 3Kisha tuende tukamate Sanduku la Agano la Mungu wetu, maana hatukulijali wakati wa utawala wa mufalme Saulo.” 4Watu wote wakakubaliana na pendekezo lile maana waliliona kuwa jambo jema.
5Kwa hiyo, Daudi akawakusanya Waisraeli wote katika inchi, tokea kwenye kijito cha Sihori kinachokuwa Misri, mpaka kwenye kiingilio cha Hamati kwa kulileta Sanduku la Agano toka Kiriati-Yearimu. #Ang. 1 Sam 7.1-2 6Daudi akiandamana na Waisraeli wote, akaenda mpaka katika muji wa Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu, katika inchi ya Yudea, kwa kulitwaa toka kule Sanduku la Agano linaloitwa kwa jina la Yawe anayeikaa kwenye kiti chake cha kifalme juu ya makerubi. #Ang. Kut 25.22 7Basi, wakalitwaa Sanduku la Agano kutoka katika nyumba ya Abinadabu wakilibeba juu ya gari jipya. Uza na Ahio wakaongoza gari lile. 8Daudi na Waisraeli wote wakakuwa wanacheza kwa nguvu zao zote, mbele ya Mungu. Waliimba nao wakikuwa wanapiga ala za muziki zilizotengenezwa kwa muti wa muvinje: vinubi, vinanda, matari, matoazi na baragumu.
9Walipofika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Kidoni, Uza akaunyoosha mukono wake kwa kuzuia Sanduku la Agano kwa sababu ngombe walijikwaa. 10Mara moja Yawe akamukasirikia Uza kwa kuligusa sanduku, akamwua. Uza akakufa palepale mbele ya Mungu. 11Daudi akakasirika kwa sababu Yawe alimwua Uza akiwa na hasira. Kwa sababu hiyo, pahali pale panaitwa Pigo la Uza mpaka leo.
12Siku hiyo Daudi akamwogopa Mungu, akasema: “Sasa, nitaweza namna gani kupeleka Sanduku la Agano katika nyumba yangu?” 13Basi, Daudi hakupeleka sanduku mpaka katika muji wa Daudi,#13.13 muji wa Daudi: ni kusema: Yerusalema. lakini akalipeleka katika nyumba ya Obedi-Edomu wa Gati. 14Sanduku lile la Mungu lilikaa kule kwa Obedi-Edomu kwa muda wa miezi mitatu, naye Yawe akabariki nyumba ya Obedi-Edomu na mali yake yote. #Ang. 1 Sik 26.4-5
Currently Selected:
1 Mambo ya Siku 13: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.