YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 100

100
Nchi zote zaitwa kumsifu Mungu
Zaburi ya Shukrani.
1Mshangilieni BWANA, enyi nchi zote;
2Mtumikieni BWANA kwa furaha;
Njoni mbele zake mkiimba;
3 # Ayu 10:8,9; Mhu 12:1; Efe 2:10; Eze 34:30 Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.
4Ingieni malangoni mwake kwa shukrani;
Nyuani mwake kwa kusifu;
Mshukuruni, lihimidini jina lake;
5 # 1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 106:1; 107:1; 118:1; 136:1; Yer 33:11 Maana BWANA ni mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Currently Selected:

Zaburi 100: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy