YouVersion Logo
Search Icon

Zab 23

23
Mchungaji Mwema
Zaburi ya Daudi.
1 # Yn 10:11; 1 Pet 2:25 BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
2 # Ufu 7:17; Eze 34:14 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 # Zab 46:11; Isa 8:10; Zek 8:23; Mt 1:23; Mdo 18:9,10 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
5Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.
6 # 2 Kor 5:1 Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Currently Selected:

Zab 23: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy