YouVersion Logo
Search Icon

Lk 1:26, 27, 28, 29, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37, 38, 39, 40, 41, 42, 43, 44, 45, 46, 47, 48, 49, 50, 51, 52, 53, 54, 55, 56

Lk 1:28 SUV

Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.

Lk 1:29 SUV

Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?

Lk 1:30 SUV

Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

Lk 1:31 SUV

Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

Lk 1:33 SUV

Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

Lk 1:34 SUV

Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?

Lk 1:37 SUV

kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.

Lk 1:40 SUV

akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.

Lk 1:43 SUV

Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?

Lk 1:45 SUV

Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.

Lk 1:46 SUV

Mariamu akasema, Moyo wangu wamwadhimisha Bwana

Lk 1:47 SUV

Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu

Lk 1:49 SUV

Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu.

Lk 1:50 SUV

Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha.

Lk 1:51 SUV

Amefanya nguvu kwa mkono wake; Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao

Lk 1:52 SUV

Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; Na wanyonge amewakweza.

Lk 1:53 SUV

Wenye njaa amewashibisha mema, Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.

Lk 1:54 SUV

Amemsaidia Israeli, mtumishi wake; Ili kukumbuka rehema zake

Lk 1:55 SUV

Kama alivyowaambia baba zetu, Ibrahimu na uzao wake hata milele.

Lk 1:56 SUV

Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy