YouVersion Logo
Search Icon

Yn 1:2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 17, 18

Yn 1:2 SUV

Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

Yn 1:3 SUV

Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

Yn 1:4 SUV

Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.

Yn 1:5 SUV

Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.

Yn 1:6 SUV

Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.

Yn 1:7 SUV

Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.

Yn 1:8 SUV

Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.

Yn 1:9 SUV

Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.

Yn 1:10 SUV

Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.

Yn 1:11 SUV

Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.

Yn 1:12 SUV

Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake

Yn 1:16 SUV

Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.

Yn 1:17 SUV

Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy