Zaburi 30
30
Zaburi 30
Maombi ya shukrani
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi.
1 Nitakutukuza wewe, Ee Bwana,
kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi,
na hukuacha adui zangu
washangilie juu yangu.
2 Ee Bwana Mungu wangu, nilikuita unisaidie
na wewe umeniponya.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu#30:3 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, yaani Shimo lisilo na mwisho.,
umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti.
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake;
lisifuni jina lake takatifu.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,
bali upendo wake hudumu siku zote.
Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha,
lakini furaha huja asubuhi.
6 Nilipofanikiwa nilisema,
“Sitatikiswa kamwe.”
7 Ee Bwana, uliponijalia,
uliuimarisha mlima wangu,
lakini ulipouficha uso wako
nilifadhaika.
8Kwako wewe, Ee Bwana, niliita,
niliomba rehema kwa Bwana:
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu,
katika kushuka kwangu shimoni?
Je, mavumbi yatakusifu?
Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia;
Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza,
ulinivua gunia ukanivika shangwe,
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya.
Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Currently Selected:
Zaburi 30: NEN
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.