Zaburi 26
26
Zaburi 26
Maombi ya mtu mwema
Zaburi ya Daudi.
1 Ee Bwana, nithibitishe katika haki,
maana nimeishi maisha yasiyo na lawama;
nimemtumainia Bwana
bila kusitasita.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime,
uuchunguze moyo wangu
na mawazo yangu;
3 kwa maana upendo wako
uko mbele yangu daima,
nami natembea siku zote
katika kweli yako.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu,
wala siandamani na wanafiki,
5 ninachukia kusanyiko la watenda maovu,
na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia,
naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa,
huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako unakoishi,
mahali pale utukufu wako hukaa.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi,
wala uhai wangu pamoja na wanaomwaga damu,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu,
ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama;
nikomboe na unihurumie.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare;
katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Currently Selected:
Zaburi 26: NEN
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.