YouVersion Logo
Search Icon

Obadia Utangulizi

Utangulizi
Maana ya jina Obadia ni “Mtumishi wa Yehova.” Hakuna habari zinazojulikana kuhusu huyu nabii isipokuwa mambo yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Obadia alitoa unabii kuhusu hukumu ya Mungu dhidi ya taifa la Edomu, kukomeshwa na kuangamizwa kwalo lisiwepo tena ulimwenguni. Waedomu, waliokuwa uzao wa Esau, walijivunia usalama katika ngome zao zilizokuwa Mlima Seiri, kusini mwa Bahari ya Chumvi. Waliwatazama watu wa Yuda walipopatwa na mikasa mikononi mwa wavamizi bila kuwasaidia. Mwanzoni mwa karne ya tisa Waedomu wenyewe walishiriki zaidi ya mara nne kuiteka nyara Yerusalemu.
Mwandishi
Obadia.
Kusudi
Kuonyesha kwamba Mungu anawahukumu wale wanaowadhuru watu wake.
Mahali
Yerusalemu.
Tarehe
Kati ya 605–586 K.K.
Wahusika Wakuu
Waedomu.
Wazo Kuu
Obadia alitangaza hukumu ya Mungu dhidi ya Waedomu, na akatabiri kuangamizwa kwao na kufutwa kwa kumbukumbu lao katika uso wa dunia. Wale wanaopigana na watu walioitwa na Mungu, yeye hupigana nao na kufuta kumbukumbu lao duniani wasipotubu.
Mambo Muhimu
Hukumu ya Mungu, na kuangamizwa kwa taifa la Waedomu.
Mgawanyo
Maangamizi ya Edomu (1-14)
Kurejezwa kwa Israeli (15-21).

Currently Selected:

Obadia Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy