YouVersion Logo
Search Icon

Esta Utangulizi

Utangulizi
Kitabu hiki kinachukua jina la mhusika wake mkuu, Esta. Jina hili limetokana na neno la Kiajemi ambalo maana yake ni “Nyota.” Jina la Esta la Kiebrania ni “Hadassah,” maana yake “Mhadasi” ambayo ni aina ya miti iliyokuwa inastawi milimani karibu na Yerusalemu, na ilikuwa inatumika kujengea vibanda wakati wa Sikukuu ya Vibanda. Kitabu hiki kinaelezea kisa cha msichana mzuri wa Kiyahudi ambaye Mfalme Ahasuero wa Kwanza alimchagua awe malkia wake.
Matukio yaliyowapata Wayahudi yanayoelezewa kwenye kitabu hiki yalitukia huko Shushani, uliokuwa mji mkuu wa Uajemi wakati wa Mfalme Ahasuero, aliyetawala Uajemi kuanzia 486–465 K.K. Kule kuokolewa kwa Wayahudi kwa ajabu wakati wa Mfalme Ahasuero baadaye kuliadhimishwa kila mwaka kama Sikukuu ya Puri; wakati huu, kitabu cha Esta husomwa hadharani.
Mwandishi
Ingawa mwandishi hajulikani kwa wazi, inawezekana akawa Mordekai. Wengine hudhani ni Ezra au Nehemia kwa sababu ya mtindo wa kuandika.
Kusudi
Kuonyesha ukuu wa Mungu, na upendo wake kwa watu wake.
Mahali
Katika jumba la kifalme huko Shushani, mji mkuu wa Uajemi.
Tarehe
Kinadhaniwa kuandikwa mwaka wa 470 K.K.
Wahusika Wakuu
Esta, Mordekai, Mfalme Ahasuero, na Hamani.
Wazo Kuu
Mungu aliwaokoa Wayahudi katika maangamizi yaliyopangwa na Hamani. Mungu aligeuza mabaya yaliyokusudiwa dhidi ya Wayahudi yakawapata adui zao katika utawala wote wa Mfalme Ahasuero, baada ya Esta na watu wake kumwomba Mungu.
Mambo Muhimu
Esta kuchaguliwa kuwa malkia badala ya Vashti aliyekuwa malkia mbele yake, na vile Mungu alivyobadilisha makusudi ya Hamani dhidi ya Wayahudi.
Mgawanyo
Esta afanywa malkia (1:1–2:23)
Hila ya Hamani kuwaangamiza Wayahudi (3:1–5:14)
Ushindi wa Wayahudi (6:1–10:3).

Currently Selected:

Esta Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy