YouVersion Logo
Search Icon

2 Wafalme Utangulizi

Utangulizi
Kwa kuwa kitabu cha 1 Wafalme na hiki cha 2 Wafalme ni historia moja inayoendelea, taarifa za msingi kwa ajili ya kitabu hiki cha 2 Wafalme ziko katika utangulizi wa 1 Wafalme.
Mwandishi
Mwandishi wa kitabu hiki hajulikani, lakini mapokeo ya Kiyahudi yanasema ni nabii Yeremia, au kikundi cha manabii.
Kusudi
Kuonyesha yale yatakayowakuta wale wanaokataa kumfanya Mungu kuwa kiongozi wao wa kweli.
Mahali
Katika nchi ya Israeli.
Tarehe
Hakuna uhakika ni wakati upi hiki kitabu kiliandikwa.
Wahusika Wakuu
Eliya, Elisha, mwanamke Mshunami, Naamani, Yezebeli, Yehu, Yoashi, Hezekia, Senakeribu, Isaya, Manase, Yosia, Yehoyakimu, Sedekia, na Nebukadneza.
Wazo Kuu
Kuanguka kwa falme zote mbili za Israeli na Yuda kulisababishwa na kutokutii maagizo ya Mungu, na kuishi maisha ya dhambi. Hali hii iliwasababisha kuwa mateka na kukaa utumwani, nayo miji yao ikaharibiwa, hii ikiwa ni hukumu kutoka kwa Mungu.
Mambo Muhimu
Kitabu hiki kinaandika majanga mawili makubwa yaliyosababisha kuanguka kwa Israeli na Yuda:
1. Kuharibiwa kwa mji mkuu wa Israeli, yaani Samaria, na taifa kuchukuliwa kwenda utumwani;
2. Kuharibiwa kwa Yerusalemu, na Yuda kupelekwa utumwani.
Mgawanyo
Eliya na Elisha (1:1–8:15)
Wafalme wa Israeli na wa Yuda (8:16–17:6)
Israeli wachukuliwa mateka kwenda Ashuru (17:7–23:37)
Kuanguka kwa Yerusalemu (24:1–25:30).

Currently Selected:

2 Wafalme Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy