YouVersion Logo
Search Icon

2 Yohana Utangulizi

Utangulizi
Waraka wa pili wa Yohana uliandikwa kwa bibi mteule na watoto wake. Unaweza kuwa ulimhusu mtu binafsi na jamaa yake, au ulilihusu kanisa fulani. Msisitizo unawekwa katika umuhimu wa imani kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu katika umbo la mwanadamu. Inawapasa waumini wanaosoma kudumu katika pendo la Mungu, na kukataa mafundisho mapotovu yanayopinga imani ya kweli.
Yohana pia anaandika kuwaonya ili waweze kutambua walimu wa uongo waliosafiri huku na huko, wasije wakawaunga mkono na kuwasaidia. Yaani mtu yeyote asije akachangia kwenye kueneza mafundisho ya uongo badala ya yale ya kweli.
Mwandishi
Mtume Yohana.
Kusudi
Kuhimiza mwenendo wa muumini, na maonyo kuhusu wadanganyifu na mbinu zao.
Mahali
Efeso.
Tarehe
Kama mwaka wa 90 B.K.
Wahusika Wakuu
Yohana, bibi mteule na watoto wake.
Wazo Kuu
Mtume Yohana anaagiza watu kuenenda katika kweli na kumtii Mungu, wakijihadhari na udanganyifu, ili wapate kumpenda Mungu, na kupendana wao kwa wao.
Mambo Muhimu
Pendo la kweli ni kuwajali wengine. Tunatamani kupendwa na kuwapenda wengine, lakini tunaona mifano michache sana ya uhalisi katika jambo hili. Dunia imejaa ubinafsi, uchoyo na kujipenda mwenyewe.
Mgawanyo
Salamu (1-3)
Ushauri na maonyo (4-11)
Hitimisho (12-13).

Currently Selected:

2 Yohana Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy