1
Marko 7:21-23
Biblia Habari Njema
BHN
Maana kutoka ndani, moyoni mwa mtu, hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, uchoyo, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi na upumbavu. Maovu hayo yote yatoka ndani ya mtu, nayo humtia mtu unajisi.”
Compare
Explore Marko 7:21-23
2
Marko 7:15
Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mtu kutoka nje kinachoweza kumtia mtu unajisi. Lakini kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia mtu unajisi.”
Explore Marko 7:15
3
Marko 7:6
Yesu akawajibu, “Wanafiki nyinyi! Nabii Isaya alitabiri sawa kabisa juu yenu alipoandika: ‘Mungu asema: Watu hawa, huniheshimu kwa maneno tu, lakini mioyoni mwao, wako mbali nami.
Explore Marko 7:6
4
Marko 7:7
Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu.’
Explore Marko 7:7
5
Marko 7:8
Nyinyi mnaiacha amri ya Mungu na kushikilia maagizo ya watu.”
Explore Marko 7:8