1
Waroma 6:23
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.
Compare
Explore Waroma 6:23
2
Waroma 6:14
Kwa maana hamutatawaliwa tena na zambi, kwa sababu hamuishi chini ya uongozi wa Sheria lakini chini ya uongozi wa neema ya Mungu.
Explore Waroma 6:14
3
Waroma 6:4
Hivi, kwa njia ya ubatizo, tuliungana naye katika kufa na katika kuzikwa kwake, kusudi kama vile Kristo alivyofufuliwa kwa uwezo wenye utukufu wa Baba, sisi vilevile tupate kuishi katika maisha mapya.
Explore Waroma 6:4
4
Waroma 6:13
Musitoe tena viungo vya mwili wenu kufanya zambi, mukivitumikisha kama vyombo vya kufanya mabaya. Lakini mujitoe wenyewe kwa kumutumikia Mungu kama watu waliofufuliwa na mutumikishe viungo vya mwili wenu kama vyombo vya kufanya haki.
Explore Waroma 6:13
5
Waroma 6:6
Kwa maana tunajua kwamba ule utu wetu wa zamani ulitundikwa pamoja na Kristo, kusudi tusitawaliwe tena na hiyo tabia ya zambi na tusikuwe tena watumwa wa zambi.
Explore Waroma 6:6
6
Waroma 6:11
Hivi vilevile mujihesabu kuwa mumekufa kwa ajili ya zambi na kuwa munaishi pamoja na Mungu mukiungana na Yesu Kristo.
Explore Waroma 6:11
7
Waroma 6:1-2
Basi sasa tuseme nini? Tuendelee kuishi katika zambi kusudi neema ya Mungu izidi kuongezeka? Hapana hata kidogo! Sisi tuliokufa kwa ajili ya zambi, namna gani tutaweza tena kuishi katika zambi?
Explore Waroma 6:1-2
8
Waroma 6:16
Munajua hakika kwamba mukijitoa wenyewe kwa mutu fulani kuwa watumwa wake na kulazimishwa kumutii, munakuwa kweli watumwa wa yule munayemutii. Ikiwa ni utumwa wa zambi, mwisho wake ni kifo; ikiwa ni kumutii Mungu, mwisho wake ni maisha ya haki.
Explore Waroma 6:16
9
Waroma 6:17-18
Lakini asante kwa Mungu, kwa maana ninyi muliokuwa zamani watumwa wa zambi mumetii sasa kwa moyo wenu wote kanuni za mafundisho muliyopewa. Mumewekwa kuwa huru toka katika utumwa wa zambi, na sasa mumegeuka watumwa wa haki.
Explore Waroma 6:17-18
Home
Bible
Plans
Videos