1
Ufunuo 3:20
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.
Compare
Explore Ufunuo 3:20
2
Ufunuo 3:15-16
Ninajua matendo yako: wewe si baridi wala si moto. Afazali ungekuwa baridi tu au moto tu. Lakini sasa kwa sababu wewe ni mwenye uvuguvugu, ni kusema hauko baridi wala moto, nitakutapika kutoka katika kinywa changu.
Explore Ufunuo 3:15-16
3
Ufunuo 3:19
Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.
Explore Ufunuo 3:19
4
Ufunuo 3:8
Ninajua matendo yako. Ninajua kwamba wewe hauna uwezo mwingi, lakini umeshika neno langu, nawe haukukana jina langu. Basi nimefungua mulango wazi mbele yako, wala hakuna anayeweza kuufunga.
Explore Ufunuo 3:8
5
Ufunuo 3:21
Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.
Explore Ufunuo 3:21
6
Ufunuo 3:17
Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.
Explore Ufunuo 3:17
7
Ufunuo 3:10
Kufuatana na vile ulivyojichunga katika uvumilivu sawa nilivyokuagiza, mimi vilevile nitakuchunga na hasara wakati itakapokuja katika dunia yote kwa kuwajaribu wakaaji wake.
Explore Ufunuo 3:10
8
Ufunuo 3:11
Ninakuja upesi. Shika sana kile unachokuwa nacho, kusudi mutu yeyote asinyanganye taji yako ya ushindi.
Explore Ufunuo 3:11
9
Ufunuo 3:2
Amuka! Uimarishe kile kinachobaki kinachokaribia kufa, kwa maana nimeona kwamba matendo yako si makamilifu mbele ya Mungu wangu.
Explore Ufunuo 3:2
Home
Bible
Plans
Videos