1
Ufunuo 12:11
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.
Compare
Explore Ufunuo 12:11
2
Ufunuo 12:10
Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.
Explore Ufunuo 12:10
3
Ufunuo 12:9
Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.
Explore Ufunuo 12:9
4
Ufunuo 12:12
Kwa sababu hii, ninyi munaokaa mbinguni, nayo mbingu kwa jumla, mushangilie! Ole kwenu ninyi munaokaa katika dunia na katika bahari kwa maana yule Mwovu ameshuka kwenu, naye anajaa na hasira, kwa sababu anajua kwamba wakati unaomubakilia ni mudogo.”
Explore Ufunuo 12:12
5
Ufunuo 12:7
Halafu kukatokea vita katika mbingu. Mikaeli na wamalaika zake wakapigana na yule nyoka mukubwa. Naye yule nyoka akapigana nao pamoja na wamalaika zake
Explore Ufunuo 12:7
6
Ufunuo 12:17
Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.
Explore Ufunuo 12:17
7
Ufunuo 12:1-2
Kisha kukaonekana kitambulisho kikubwa mbinguni. Kulikuwa mwanamuke aliyekuwa amefunikwa na jua, na mwezi chini kwenye miguu yake. Na juu ya kichwa kulikuwa taji lenye nyota kumi na mbili. Mwanamuke yule alikuwa mimba, naye alikuwa akilia kwa sababu ya uchungu na maumivu ya kuzaa.
Explore Ufunuo 12:1-2
8
Ufunuo 12:5-6
Halafu yule mwanamuke akazaa mutoto mwanaume atakayetawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Lakini mutoto yule akanyanyuliwa na kupelekwa kwa Mungu kwenye kiti chake cha kifalme. Na yule mwanamuke akakimbilia katika jangwa kwenye nafasi Mungu aliyomutayarishia kusudi apate kulishwa kule kwa muda wa siku elfu moja mia mbili makumi sita.
Explore Ufunuo 12:5-6
9
Ufunuo 12:3-4
Kisha kukaonekana kitambulisho kingine mbinguni. Kulikuwa nyoka mukubwa mwekundu mwenye vichwa saba na pembe kumi. Juu ya kila kichwa kulikuwa taji saba. Mukia wake ulikokota sehemu moja ya tatu ya nyota za mbingu na kuzitupa katika dunia. Yule nyoka akasimama mbele ya yule mwanamuke aliyekuwa tayari kuzaa, kusudi amumeze mutoto wakati atakapozaliwa.
Explore Ufunuo 12:3-4
10
Ufunuo 12:14-16
Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu. Basi yule nyoka akatokeza maji kwa uwingi ndani ya kinywa chake, nayo yakatelemuka kama muto nyuma ya yule mwanamuke kusudi yapate kumupeleka. Lakini udongo ukamusaidia yule mwanamuke; ukabomoka kama vile kinywa na kumeza ule muto uliotoka katika kinywa cha yule nyoka.
Explore Ufunuo 12:14-16
Home
Bible
Plans
Videos