1
Zaburi 37:4
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.
Compare
Explore Zaburi 37:4
2
Zaburi 37:5
Umutolee Yawe maisha yako, umutumainie yeye, naye atakufanyia kitu.
Explore Zaburi 37:5
3
Zaburi 37:7
Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.
Explore Zaburi 37:7
4
Zaburi 37:3
Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.
Explore Zaburi 37:3
5
Zaburi 37:23-24
Yawe anaongoza mutu katika njia yake, anamulinda yule anayemupendeza. Hata akianguka, hatabaki chini, kwa sababu Yawe anamuimarisha.
Explore Zaburi 37:23-24
6
Zaburi 37:6
Ataifanya haki yako iangae kama mwangaza wa jua muchana kati.
Explore Zaburi 37:6
7
Zaburi 37:8
Usiwake hasira wala kuwa na kasirani; usihangaike, maana hiyo inazidisha ubaya.
Explore Zaburi 37:8
8
Zaburi 37:25
Nilikuwa kijana na sasa mimi ni muzee; hata kidogo sijaona mutu wa haki ameachwa na Mungu, au watoto wake wakiombaomba chakula.
Explore Zaburi 37:25
9
Zaburi 37:1
Zaburi ya Daudi. Usihangaike kwa sababu ya waovu; usiwaonee wivu wanaotenda mabaya.
Explore Zaburi 37:1