Wandugu zangu, sihesabu kwamba nimekwisha kupokea zawadi, lakini ninafanya jambo moja tu: ninasahau yanayokuwa nyuma, nikifukuzia yanayokuwa mbele yangu. Kwa hiyo ninakaza mwendo mpaka mwisho nipate kupokea ile zawadi Mungu aliyotuitia katika mbingu kwa njia ya Yesu Kristo.