Yesu akamujibu: “Amri ya kwanza katikati ya zote ni hii: ‘Sikia, wewe taifa la Waisraeli! Bwana Mungu wetu ndiye Bwana peke yake. Umupende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili yako yote na kwa nguvu yako yote.’ Na amri ya pili ni hii: ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’ Hakuna amri zingine kubwa kupita hizi.”