Kama ilivyokuwa katika siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi. Kwa maana katika siku zile mbele ya kunyesha kwa mvua kubwa, watu walikuwa wakikula na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka ilipotimia siku ile Noa alipoingia ndani ya chombo. Nao hawakutambua kitu mpaka mvua kubwa sana ilipotokea, na kuwaua wote. Na ni hivi itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi.