Mungu anaongea na watu katika ndoto na maono,
wakati usingizi muzito unapowapata,
wanaposinzia katika vitanda vyao.
Halafu anawafungua watu masikio yao;
anawatia hofu kwa maonyo yake,
wapate kuachana na matendo yao mabaya,
na kuvunja kiburi chao.
Hivyo anamukinga mutu asiangamie katika shimo,
maisha yake yasiangamie kwa upanga.