Na sasa Yawe ametimiza jambo hilo na kutenda kama alivyosema. Kwa sababu ninyi wote mulimukosea Yawe na kukataa kumutii, jambo hilo limewapata. Basi! Leo ninafungua minyororo toka mikono yako. Kama unaona ni vizuri kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi tuende pamoja; mimi nitakutunza vizuri. Lakini kama unaona si vizuri kwako kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi, usikuje. Ujue kwamba unaweza kwenda popote katika inchi hii. Basi kwenda kwenye unaona ni vizuri kwenda.