Bwana wangu mufalme, watu hawa wamefanya kitu kibaya. Wamemutia yule nabii Yeremia katika kisima ambamo kwa kweli atakufa kwa njaa, kwa maana hakuna chakula tena katika muji. Halafu mufalme akamwamuru yule Mwetiopia Ebedimeleki hivi: Twaa watu watatu kutoka hapa uende umutoe nabii Yeremia katika kisima, mbele hajakufa.