Utawaambia hivi:
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Alaaniwe mutu yeyote asiyeshika masharti ya agano hili. Hili ni agano nililowaagiza babu zenu kutii nilipowaondoa katika inchi ya Misri, kutoka katika shimo la moto. Niliwaambia wanitii na kufanya yote niliyowaamuru, na kwamba wakifanya hivyo, watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.