1
Isaya 6:8
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi.
Compare
Explore Isaya 6:8
2
Isaya 6:3
Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake.
Explore Isaya 6:3
3
Isaya 6:5
Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.
Explore Isaya 6:5
4
Isaya 6:1
Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote
Explore Isaya 6:1
5
Isaya 6:7
Naye akinigusa nalo kwenye mudomo, akasema: Kaa hili limekugusa kwenye mudomo; umeondolewa kosa lako, umesamehewa zambi yako.
Explore Isaya 6:7
6
Isaya 6:2
na juu yake kulikuwa kumeikaa wamalaika. Kila mumoja alikuwa na mabawa sita: mawili kwa kufunika uso, mawili kwa kufunika mwili na mawili ya kuruka.
Explore Isaya 6:2
7
Isaya 6:6
Basi, mumoja wa hao wamalaika akaruka na kunifikia, akiwa ameshika katika mukono koleo lililokuwa na kaa la moto alilolitwaa kwenye mazabahu.
Explore Isaya 6:6
8
Isaya 6:9
Naye akaniambia: Kwenda kuwaambia watu hawa hivi: Mutasikiliza sana, lakini hamutaelewa; mutaangalia sana, lakini hamutaona.
Explore Isaya 6:9
9
Isaya 6:10
Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.
Explore Isaya 6:10